Baada ya kuona kuwa amesalitiwa Shani anaamua 'kumwaga mboga'. Anapenyeza taarifa kwa Jeshi la Polisi; taarifa zinaloliwezesha jeshi hilo Jiji Dar es Salaam kukamata shehena ya dawa za kulevya iliyoingizwa nchini. Dili imetibuka wahusika wameingia mitini.
Saa chache kabla ya uteketezaji kufanyika bohari ilikohifadhiwa shehena hiyo ya dawa haramu inavamiwa; baadhi ya askari polisi waliokuwa wakilinda wanauawa na shehena inatoweka. Sam Kabuto, Inspekta wa Polisi aliyekuwa likizo anarejeshwa kazini kufuatia tukio hili. Unaanzaa msako mkali. Sam yuko mbioni kuusambaratisha mtandao na kuwatia mbaroni watuhumiwa. Hii inachochea hasira kali miongoni mwa wahalifu hao. Wanajiapiza kulipiza kisasi lakini kadri wanavyojaribu ndivyo wanavyozidi kuchemka na kiu yao ya kulipa kisasi ndivyo inavyoongezeka.