Saa yako kufika haimaanishi saa katika damu na nyama, kama vile saa saba mchana au saa ya kula chakula bali inamaanisha saa katika ulimwengu wa roho. Saa ni kipimo cha muda, katika ulimwengu wa mwili na ulimwengu wa roho pia, lakini katika ulimwengu wa roho saa inasomwa kutokana na matukio. Kwa mfano, watu wanaweza kusema huyu amepona ajali mbaya kwa sababu saa yake haijafika.
Na ninaposema mambo ya kufanya saa yako ikifika siyo lazima iwe saa ya kufa kwako lakini saa au siku ya kufikwa na jambo fulani ambalo limekuwa likisubiriwa katika ulimwengu wa roho. Saa yako ikifika katika ulimwengu wa roho huwa ni kama mtihani pia. Ukivuka kwa ufaulu unaenda kiwango kingine cha juu zaidi na ngazi njema zaidi katika Kristo Yesu. Katika kitabu hiki utajifunza mambo ya kufanya ili uweze kufaulu mtihani wako saa yako ikifika.