Mbinu za Kupata Mume Mwema ni kitabu kilichoandikwa ili kumsaidia binti au mwanamke wa Kikristo ambaye yuko tayari kujihusisha na mahusiano na mwanaume ili kuyakuza mahusiano na upendo wao hadi kufikia kufunga ndoa.
Kitabu hiki kimeandikwa na mwanaume kwa hiyo kinakupa mbinu za kushinda changamoto za mahusiano- uchumba na ndoa, kutoka katika macho ya mwanaume. Ukisoma kitabu hiki utajua ni vitu gani ambavyo wanawake wanakosea katika mahusiano ya awali na uchumba na utajua ni mambo gani ufanye ambayo yatamfanya mwanaume akuone unafaa kuchumbiwa.
Kitabu hiki kinaongelea hatua za awali kuanzia mnakutana mara ya kwanza na anakuomba namba ya simu mpaka inafika anaamua kukuchumbia ni mbinu gani zitakutofautisha na mabinti wengine wenye sifa za kuchumbiwa na mtu huyo huyo unayetamani akuchumbie wewe. Kama unataka mwaka usiishe uwe umeshachumbiwa ingawa sasa hivi huna hata boyfriend basi soma kitabu hiki leo na ukiweke katika matendo.