Kama tukiwa wakweli kabisa, tutakiri kwamba mara zote maisha hayajawa vile tulivyo tarajia. Kama vijana tulitarajia maisha yenye mambo makubwa na Mapenzi motomoto muda wote. Imebaki kama simulizi kwamba hayo ndo yaliyopaswa kuwa maisha yetu, uhalisia umebadili kila mpango.
Taifa la Israeli pia walikuwa na mawazo yao jinsi uhuru utakavyokuwa kutoka kwenye kifungo cha Misri na shauku kubwa juu ya kile Mungu atakachowafanyia. Kutoka 16:3 ina mambo mengi ya kutuambia kuhusu matarijio ya Waisraeli na Imani juu ya Mungu.